This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, July 17, 2012

CHADEMA WASHINGTON DC YAPATA UONGOZI MPYA

Tawi la Chadema Washington DC limepata Viongozi wapya walioshika nafasi za waliokuwa Viongozi wa muda. Katika Uchaguzi huo Cosmas Wambura amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya kuchukua nafasi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Muda Kalley Pandukizi. Nafasi ya Katibu imechukuliwa na Isidori Lyamuya aliyechukua nafasi ya Liberatus Mwang’ombe aliyekuwa Katibu. Nafasi ya Mweka hazina imechukuliwa na Ludigo Mhagama na nafasi ya katibu mwenezi imechukuliwa na Hussein Kauzella. Nafasi nyingine zilizogombewa ni Wenyeviti na Makatibu wa Mabaraza ya Vijana, Wanawake na Wazee. Pia kulikuwa na nafasi ya Afisa Habari wa Chama. Akiongea baada ya Uchaguzi Mwenyekiti aliyechaguliwa ndugu Cosmas Wambura amesema atatoa ushirikiano mkubwa katika kuendeleza shughuli mbalimbaliza kukijenga Chama. Pia Katibu mpya amesema watashirikiana na Mwenyekiti na wanachama wengine wote kuhakikisha Chama kinzidi kuwa Imara na kupata wanachama zaidi.

CHADEMA yaonya vurugu za CCM Singida


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeeleza kukerwa na vurugu za Chama cha Mapinduzi (CCM) za kuvamia mikutano yao ya hadhara mkoani hapa.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa CHADEMA ambaye pia ni mbunge wa Ubungo, John Mnyika, wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Ndago jimboni Iramba Magharibi, akisema kuwa kamwe hawatavumilia mbinu hiyo chafu ya CCM.
Alisema mbinu hiyo ya CCM kuwapiga watu mawe kwenye mkutano wa CHADEMA haivumiki na badala yake inachochea zaidi harakati ili kuikomboa nchi ambayo inakabiliwa na matatizo mengi ya kutisha yaliyochangiwa na udhaifu wa chama tawala.
Alisema wakati wowote kuanzia sasa, viongozi wa ngazi za juu wa CHADEMA watafanya ziara ya nguvu kwenye kata zote za mkoa wa Singida.
“Mmetuchokoza, hatutakubaliana na viongozi wasanii na wachumi wanaopanga mambo ya kipuuzi kama haya ya kupiga watu mawe wasio na hatia yoyote. Jiandaeni na kusanyeni mawe mengi ya kutosha, tunakuja na tutakaba kila kona,” alifafanua.
Mnyika alisema amefarijika kufika kwenye jimbo hilo linaloongozwa na Mwigulu Mchemba (CCM) kwa madai kuwa amekuwa ‘akichonga’ sana propoganda bungeni wakati hakuna chochote cha maendeleo amekifanya.
Kauli ya Mnyika ilikuja baada ya kutokea vurugu za watu kupigwa mawe kwenye mkutano huo wa hadhara na CHADEMA wamekana kuhusika na vurugu hizo zilizosababisha kifo cha mfuasi wa CCM.
Afisa wa sera na utafiti wa CHADEMA,Waitara Mwita, alisema kuwa katika mkutano huo halali, baada ya kuona hali sio nzuri za wafuasi wa CCM kuvamia mkutano huo kwa kurusha mawe na maneno ya kejeli alimpigia siku Kamanda wa Polisi kuomba ulinzi katika eneo hilo.
“Nashukuru RPC aliwasiliana na OCD na mara moja gari la polisi lilifika na askari, lakini licha ya hali kuendelea takriban mara tatu, ilitulazimu kufungua jalada polisi NDG/RB/190/2012 na tulitaja baadhi ya majina ya vijana 12, lakini OCD hakuweza kuwadhibiti vijana waliokuwa wakifanya vurugu hizo,” alisistiza Mwita.
Hata hivyo mara baada ya Waitara kuzungumza na waandishi wa habari, alifika OCD wa Wilaya ya Singida, na kumtaka kufika kwa RPC kwa mahojiano zaidi juu ya tukio hilo.

Dk. Slaa: CCM wachochezi 

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema kuwa wamebaini mpango wa makusudi unaofanywa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ndani na nje ya Bunge kwa lengo la kuwahujumu.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jioni, Dk. Slaa, alisema kuwa amelazimika kutoa tahadhari hiyo kutokana na dalili na njama alizoziona zikifanywa na CCM bungeni kupitia kwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Uchumi na Fedha, Mwigulu Mchemba, ambaye pia ni mbunge wa Iramba Magharibi.
“Leo nimemwona Mwigulu bungeni anadai eti Chedema tumefanya vurugu Singida juzi na kumuua kada wao, halafu mchana Mwenyekiti wa UVCCM wa Vyuo Vikuu, Abubakar Asenga, alizungumza na waandishi akaonyesha waraka feki na kudai ni maazimio ya Kamati Kuu ya chama chetu,” alisema Dk. Slaa.
Katibu huyo, alisisitiza kuwa CCM ndiyo waliofanya vurugu kwenye mkutano wa CHADEMA uliofanyika huko mkoani Singida na kwamba taarifa za uwepo wa vujo hizo zilikuwepo mapema lakini akashangazwa na Mwigulu, kukimbilia bungeni na kusema uongo.
Kuhusu madai ya Spika Makinda kudai kuwa amepokea majina ya wabunge wa CHADEMA wanaodaiwa kumtumia ujumbe wa vitisho Mwigullu, Dk. Slaa alisema anamshangaa kwa kuligeuza Bunge kuwa mahakama na hivyo, akashauri kuwa madai hayo lazima yaripotiwe polisi si bungeni.
“Sasa hizi ni mbinu zimeandaliwa kwa kuwakodi watu kufanya vurugu kwenye mikutano yetu na kueneza maneo ya uchochezi ili CHADEMA tuonekane ni chama cha vujo. Nimeseme kwamba hatuko tayari kufanyiwa mchezo huo na hao wanaotumika kufanya hivyo waache mara moja,” alionya.
Kuhusu waraka uliosambazwa jana na Asenga, ukidaiwa ni maazimio ya CC ya CHADEMA ya hivi karibuni unaokihusisha na kuchochea mgomo wa madaktari na ule wa walimu unaofukuta, Dk. Slaa, alisema kuwa aliyeuandaa ni mpumbavu kwa vile mambo yaliyoandikwa humo yanaihusu CCM.
“Kwanza wewe ni shahidi na mchango wa Mwigulu bungeni kila mtu anaufahamu, sasa leo kuandika waraka wa kijinga kama huu ukisema CHADEMA inataka kumdhoofisha kwa kuwa ni mtetezi makini wa watu, napata shida sana huyu ana umakini gani na amemtetea nani bungeni,” alihoji Dk. Slaa.
Mbali na mengi aliyozungumza kuhusu waraka huo, Dk. Slaa alishangazwa kuona ukihusishwa kuwa umetoka kwake lakini hakuna saini ya kuonyesha ukweli kuwa aliiandika yeye badala yake limewekwa jina na salamu ambayo si ya CHADEMA.
“Sisi salamu yetu ni ‘People’s Power’…hiyo ya Idumu Nguvu ya Umma, iliyotumika kwenye waraka huo ni dhahiri kuwa imetoka CCM kwani wao husalimiana ‘Kidumu Chama cha Mapinduzi’. Mimi nyaraka zangu zote zina saini yangu na hata jina langu huwa naliandika lote kwa kirefu nikitanguliza cheo changu Dr. na si Dk. kama walivyoghushi,” alisema.

Waghushi waraka kuhusisha Chadema na migomo

Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, ameeleza kuwa wapinzani wa kisiasa wa chama hicho wameghushi waraka wenye sahihi yake ambao unakihusisha chama hicho na migomo inayoendelea nchini.

Akizungumza na NIPASHE jana kwa njia ya simu, Dk. Slaa alisema inashangaza watu kughushi waraka wa namna hiyo wakati ambao nchi inakabiliwa na changamoto nyingi hususani za kuwakwamua wananchi na lindi la umaskini.

Alisema chama hicho kitaendelea kutekeleza wajibu na majukumu yake kama chama cha siasa ikiwemo kuuelimisha umma juu ya haki za msingi pamoja na umuhimu wa kushiriki kwenye shughuli za maendeleo ya nchi.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa shirikisho la Chama Cha Mapinduzi katika Vyuo Vikuu vya Mkoa wa Dar es Salaam, Asenga Abubakar, alisambaza waraka unaodaiwa kutolewa na Dk. Slaa kwa viongozi wa Chadema kuwataka washinikize migomo nchini hususani wa walimu.

Akizungumza na NIPASHE jana, Asenga alisema waraka huo umesambazwa kwenye mitandano ya kijamii na kwamba yeye (Asenga), alitoa nakala na kuzisambaza kwa vyombo vya habari kwa nia njema ya kukemea maelekezo hayo.

TANZANIA KUTORIDHIA MISAADA YA MASHARTI KUHALALISHA USHOGA!!
Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Bernad Membe

Serikali ya Tanzania imesema iko tayari kujifunga mikanda na kujibeba yenyewe kuhakisha haikubali kudhalilishwa kiutu na utamaduni wake kwa kukubali kupokea misaada ya masharti itakayotulazimisha kukubaliana na ndoa za jinsia moja.


Kauli hiyo imetolewa bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Bernad Membe wakati akijibu swali la mbunge wa Konde Mh. Khatib Said Haji aliyetaka kujua serikali imejipanga vipi kukabiliana na janga la nchi wahisani watakapotoa misaada yao kwa lengo la kushinikiza ndoa za jinsia moja.


Akijibu swali hilo Mh. Membe amesema dini zote hapa nchini hazikubaliani na uwepo wa ndoa ya jinsia moja na viongozi wake wapo mstari wa mbele kukemea jambo hili na kwa maana hiyo utamaduni wa nchi na sheria za dini hazitambui ndoa ya jinsia moja.

Wednesday, July 11, 2012

Askari anayetuhumiwa kumteka Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka, Kamishna wa Polisi Msaidizi (ACP), Ahmed Msangi, amehojiwa na kuzungumzia kilichotokea kuhusiana na tuhuma kwamba aliambiwa arejeshe simu ya mkononi na pochi ya Dk. Ulimboka. Akizungumza, ACP Msangi alikiri kwenda katika wodi ya wagonjwa mahututi katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa nia ya kumhoji Dk. Ulimboka, ila akaeleza mshangao wake kutokana na habari zilizochapishwa mwishoni mwa wiki, kuwa aliambiwa arejeshe pochi na simu ya Dk Ulimboka kwa maana kuwa alivipora walipomteka.

Vyombo vya habari mwishoni mwa wiki vilichapisha taarifa bila kutaja jina la askari anayetuhumiwa, lakini pia ukawa unasambazwa ujumbe mfupi kupitia simu za mkononi ambao ulisema hivi:

“Kamanda Msangi aliyemkamata na kumtesa Dr. Ulimboka, yuko katika jopo la kuchunguza nini kilimtokea Dk. Ulimboka. Alipofika kumhoji Dk. Ulimboka alimwambia ‘Nirudishie simu na wallet yangu’. Kamanda Msangi taratibu akaondoka wodini kichwa chini. Kama wewe ni mpenda haki na unapinga ujinga na dhuluma, watumie ujumbe huu watu wengi kadri uwezavyo ili wamjue dhalimu aliyeongoza unyama huu,” ulisema ujumbe huo unaosambazwa kupitia simu za mkononi.

Tume ya Jeshi la Polisi iliyoundwa kuchunguza tukio la Dk. Ulimboka kutekwa nyara, kwa mujibu wa Kamanda Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, inaongozwa na Kamanda Msangi.

Kamanda Msangi azungumza
Jamhuri: Afande umetangazwa kuongoza hii Tume ya Polisi kuchunguza suala la Dk. Ulimboka, lakini taarifa zilisosambaa zinaonyesha Ulimboka alikwambia umerejeshee simu na wallet yake. Unalizungumziaje hili?

Kamanda Msangi: Hata mimi nimesikia hizi taarifa, na zimenisikitisha mno. Naamini taarifa hizi zina malengo ya ziada. Si kweli kwamba nilishiriki kumteka Dk. Ulimboka na wala sijawahi kuwa na wazo hilo.

Jamhuri: Ikiwa hukushiriki kumteka iweje wodini akwambie nirudishie simu yangu?

Msangi: Kwanza ifahamike mimi huyu Dk. Ulimboka na mwenzake Dk. Deo nimewafahamu siku nyingi sana. Kwa maana hiyo ni mtu anayenifahamu vizuri tu. Kuna upotoshaji wa makusudi umefanywa ambao mimi nadhani una msukumo wa kisiasa.

Alichosema Dk. Ulimboka nilipozungumza naye, ni kwamba simu moja ilidondoka, nyingine wale watu waliomteka wameichukua pamoja na wallet yake. Hivyo alikuwa ananitajia vitu vilivyopotea. Nilipomuuliza iwapo anakumbuka namba ya simu, aliniambia nikamuulize Dk. Deo. Sasa nashangaa mtu aliyepenyeza uongo huu kwamba alisema mimi ndiye niliyempora hivyo vitu… sielewi ni nani na ana malengo gani.

Jamhuri: Haya unayasema wewe, hivi unadhani jamii itakuamini kwa kauli hizi, haitaonekana unajitetea tu?

Msangi: Wakati anazungumza maneno haya, alikuwapo Profesa Museru ambaye ni Mkurugenzi wa MOI. Sina cha kuficha kamuulize tu, atakwambia alichosema Dk. Ulimboka. Yupo pia Dk. Deo, huyu ananifahamu na Dk. Ulimboka anasema walikuwa wote wakati anatekwa. Dk. Deo ananifahamu, akaulizwe iwapo mimi ndiye niliyemteka Dk. Ulimboka.

Jamhuri: Tuhuma hizi zilianza kusambaa mapema tu Ijumaa. Je, wewe hukuwa na hofu kwenda pale MOI kumhoji Dk. Ulimboka?

Msangi: Ndugu yangu, nchi hii ina askari wengi mno. Hivi mimi kwa akili ya kawaida naweza kushiriki kumteka Dk. Ulimboka kisha nikaenda wodini kumhoji? Hata katika akili ya kawaida ya binadamu hilo haliwezekani.

Jamhuri: Hizi tuhuma zilizoelekezwa kwako ni nzito. Wewe ndiye uliyeteuliwa kuongoza Tume ya Uchunguzi wa tatizo hili. Je, unadhani uchunguzi utakaofanya utaaminiwa na wananchi ukitoa ripoti?

Msangi: Mimi ninachokuhakikishia sikushiriki kumteka na si kweli kwa kila hali. Mambo kama haya yanakatisha tamaa. Kama tunaanza kuzushiana uongo kwa kiwango hiki, nchi hii sijui inaelekea wapi! Kimsingi imenikatisha tamaa mno. Wapo wanaosema nijiuzulu katika Tume hii lakini mimi nasema wakubwa wangu wamenipa kazi hii na watakaloamua nitalipokea.

Hivi wewe gazeti lako likituhumiwa unaacha kuendelea kutafuta habari? Nitaendelea kufanya kazi hii kama nilivyoapa siku nilipohitimu mafunzo kwamba nitalitumikia taifa kwa uadilifu na uaminifu wa hali ya juu katika kiapo changu cha utii. Na hilo ndilo nitakaloendelea kufanya. Watu wanapenda kuharibiana maisha tu.
Profesa Museru asema alichokisikia

Mkurugenzi wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru, akizungumza na JAMHURI kuhusiana na sakata kwamba Dk. Ulimboka, alimweleza Kamanda Msangi arejeshe simu na wallet yake.

Jamhuri: Profesa nimezungumza na Kamanda Msangi juu ya tuhuma zinazomkabili kuwa aliambiwa na Dk. Ulimboka amrejeshee simu na wallet yake, na akakutaja wewe kuwa ulikuwapo wakati wa mazungumzo hayo. Wewe nini ulichokisikia kuhusiana na tuhuma hizi.

Profesa Museru: Mimi ndiye niliyempeleka pale wodini. Ni bwana mzuri tu. Nilimu-introduce (nilimtambulisha), akaanza mahojiano. Mimi hilo sikulisikia kwamba ameambiwa arejeshe simu na wallet, hilo sikulisikia.

Jamhuri: Kuna habari kuwa Kamanda Msangi baada ya kuambiwa kauli hiyo alitoweka wodini bila kuaga akikwepa kipigo kama ilivyomtokea askari mwenzake siku mbili kabla. Je, unalizungumziaje hilo profesa?

Profesa Museru: Nini? Kwamba alikimbia? Jamani nchi hii inakwenda pabaya. Mimi nilimsindikiza hadi nje ya wodi akapanda gari lake na kurejea ofisini kwake, sasa hilo la kukimbia limetokea wapi? Jamani ehee, mimi niseme katika hali kama hii sintofahamu zipo nyingi. Ni vyema kuchuja taarifa tunazozipata